emblem

Mamlaka ya Maji Safi na Usafi wa Mazingira Mjini Geita
(GEUWASA)

Huduma Zetu

FAHAMU KUHUSU MITA YA MAJI NA MATUMIZI YAKE.

Mteja anastahili kulipa bili inayotokana na matumizi yake halisi .Matumizi halisi ya mteja yanapimwa kupitia Mita ya Maji ambayo ni mali ya Mamlaka iliyofungwa katika eneo la mteja.Malipo ni kutokana na matumizi yao halisi yanayopimwa kupitia Mita zao na mita hizo za Maji humsaidia mteja kuweza kufuatilia na kudhibiti matumizi yake ya Maji .

1.Masharti ya kufungiwa mita (dira) ya maji:

• Kuanzia siku mteja atakapo fungiwa mitar, mita hiyo itakuwa chini ya dhamana yake na anapaswa kuhakikisha Usalama wake.Endapo mita itaharibiwa au kupotea mteja atalazimika kulipa gharama ya ununuzi wa mita nyingine.

• Mita (dira) ya maji itafungwa na mafundi wa Mamlaka tu.

• Mteja haruhusiwi kuifungua,kuitengeneza ,kuihamisha mahali itakapofungwa au kuruhusu watoto ama mtu mwingine yeyota kuichezea.

• Ni kosa mteja au mtu yeyote ambaye si mtumishi wa Mamlaka kufanya marekebisho yoyote katika mita na yeyote ataepatikana na kosa hilo atakatiwa Maji ikifuatiwa na hatua nyingine za kisheria.

• Mteja atawajibika kusaini mkataba wa maandishi wakati wa kufungiwa mita ya maji.Mteja atapatiwa nakala ya mkataba huo na atapaswa kuutunza na kuutoa wakati wowote utakapohitajika.