Habari
WANAWAKE GEUWASA WAUNGANA NA WENZAO KUADHIMISHA SIKU YA WANAWAKE DUNIANI.
Watumishi Wanawake wa Mamlaka ya MajiSafi na Usafi wa Mazingira Geita (GEUWASA) wameungana na wenzao kuadhimisha Siku ya Kimataifa ya Wanawake Duniani ambayo kwa Mkoa wa Geita maadhimisho hayo yamefanyika katika viwanja vya CCM Kalangalala Manispaa ya Mji Geita.
Siku hii ya Wanawake ambayo imeadhimishwa leo Machi 8 inaongozwa na kauli mbiu ya "Haki na Usawa kwa Wanawake na Wasichana, Msingi Jumuishi kufikia Dira 2050"

